Posts

KISA Cha Kusikitisha 'Baba Yangu Alisababisha Nilale na Mjomba Wangu, Kamwe Sitamsamehe'

Image
  Nimeona leo nitoe siri yangu hapa ya muda mrefu ambayo imekuwa ikiniumiza sana pale tu ninapokumbuka, nakosa raha na amani inapotea. Kwa ufupi kabisa, nilizaliwa mkoani Mara wilaya ya Musoma mjini maeneo ya Nyakato, mama yangu alibeba mimba yangu akiwa darasa sita hivyo hakumaliza shule. Ilibidi akae nyumbani mpaka pale alipojifungua, kwa wakati kulikuwa hakuna sheria kali kwa wanaowapatia wanafunzi mimba wakiwa shule. Na aliyempatia hiyo mimba naye alikuwa mwanafunzi mwenzake lkn alikuwa la saba yeye alimaliza shule. Baba yake mama ambaye ni babu yangu alikuwa na uwezo mkubwa hivyo hakushindwa kutulea mimi na mama. Nikiwa na miaka 6 ndipo nilipokuja kumjua baba yangu wakati huo nae alikuwa amekuwa mtu mzima, alikuja akanisalimia akaondoka, kwao pia walikuwa vizuri kimaisha. Nikiwa na miaka 9 naanza darasa la kwanza wakati huo tulikuwa tunaingia shule tukiwa na umri mkubwa tofauti na sasa. Mama aliolewa na mume mwingine na alikuwa ni askari jeshi, alifanikiwa kuzaa nae watoto wanne j

Mayele Hauzwi, Yanga Yaweka Masharti Maguma

Image
  UONGOZI wa Yanga umetamka kuwa mshambuliaji wao Mkongomani Fiston Mayele hayupo sokoni lakini wapo tayari kukaa meza moja kwa klabu zinazomuhitaji kwa ajili ya mazungumzo. Aliongeza kuwa kabla ya kuanza mazungumzo hayo ya Mayele na hizo klabu, kikubwa wafahamu kuwa dau la Mayele hivi sasa linafikia zaidi ya Sh 5Bil ambazo zitawashawishi wao wamuachie mshambuliaji huyo. #Yanga #Mayele #AZIZK

Majembe Saba Yaipa Kicheko Simba Katika Orodha Ya Kuwania Tuzo

Image
MAJEMBE saba yanayovuja jasho la haki ndani ya kikosi cha Simba yamewapa kicheko Simba wakiamini kuwa hawajabahatisha kupenya kwenye orodha ya kuwania tuzo bali ubora umewababe. Katika orodha ya kuwania tuzo ndani ya ligi msimu wa 2022/23 tayari Kamati ya Tuzo Tanzania iliyo chini ya Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) imetaja mastaa waliopenya kuwania tuzo zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni huku Simba ikitoa mastaa saba. Ni kwenye kipengele cha mchezaji bora ni nyota wawili wamepenya ambao ni Mzamiru Yassin na Saido Ntibanzokiza wote ni viungo. Aishi Manula maarufu kama Air Manula kipa namba moja wa timu hiyo amepenya kwenye kuwania tuzo ya kipa bora akipambana na Djigui Diarra wa Yanga na Benedict Haule wa Singida Big Stars. Watatu wamepenya kwenye tuzo ya beki bora ambao ni Shomari Kapombe, Henock Inonga na Mohamed Hussein sawa na watatu waliopenya kuwania tuzo ya kiungo bora ikiwa ni Clatous Chama, Mzamiru na Sadio. Wakati wachezaji wao wakipenya na jina la kocha Roberto Oliveir

BAADA YA KUWATAZAMA YANGA…KOCHA WA USM ALGER KANUGA WEE..KISHA AKASEMA HAYA

Image
  Kocha Mkuu wa USM Alger ya Algeria, Abdelhak Benchikha amesema hana hofu na kiwango cha Yanga na wategemee mechi ngumu zaidi ya zote zilizopita kwani wanahitaji kombe hili. “Wanatakiwa kufahamu kuwa wanakwenda kukutana na timu ya tofauti kuliko walizokutana nazo katika hatua waliyocheza,tunalihitaji hili kombe,tunaheshimu uwezo wao,” Kocha USM ALGER, Abdelhak Benchikha. Yanga atakutana na USM, Jumapili ijayo, Mei 28, 2023 katika mchezo wa kwanza wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika utakaopigwa katika Dimba la Mkapa jijini dar es Salaam na mchezo wa pili utapigwa Algeria Juni 4. USM ALger imetinga fainali ya michuano hiyo kwa kuiondoa AS FAR Rabat ya Morocco kwa jumla ya mabao 4-3 huku Yanga ikiiondoa Marumo Gallants ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 4-1.

BAADA YA KUWA ‘MNYONGE SANA’ …PHIRI KUWA CHINI YA UANGALIZI MAALUMU SIMBA

Image
  Mshambuliaji kutoka nchini Zambia Moses Phiri yupo mikononi mwa Kocha Mkuu wa Simba SC Roberto Oliveira kutokana na kupewa program maalumu itakayomrejesha kwenye ubora wake. Desemba 21, mwaka jana, Phiri alipata maumivu ya mguu kwenye mchezo dhidi ya Kagera Sugar, Uwanja wa Kaitaba walipotoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1. Baada ya hapo amekuwa nje akipambania hali yake na hata aliporejea uwanjani Februari 11, 2023 Uwanja wa General Lansana Conte dhidi ya Horoya alitumia dakika 29 alikwama kurejea kwenye hali yake ya kucheka na nyavu. Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC, Ahmed Ally amesema Phiri ana program maalumu itakayomrejesha kwenye ubora, na msimu ujao atakuwa tayari kuipambania timu. “Phiri alikuwa bado hajawa fiti baada ya kupata maumivu alipokuwa kwenye majukumu yake ya kazi ila kwa sasa ana program maalumu ambayo itamfanya arejee kwenye ubora. “Ni matumaini yetu atakuwa fiti tayari kwa kuwapa furaha Wanasimba hivyo muhimu kuwa na subra kila kitu kitakuwa sawa

KUHUSU MZIGO AMBAO SIMBA NA YANGA ZITAPA CAF…UKWELI HUU HAPA…PESA ZAONGEZWA

Image
Simba imeng’olewa hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, lakini taarifa njema kwano ni kule kuongezwa mkwanja ikijihakikisha kuvuna Dola 900,000 (zaidi ya Sh 2 Bilioni) baada ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuongeza mzigo wa fedha za zawadi kwa michuano ya msimu huu. Ongezeko hilo la fedha halijainufaisha Simba tu, bali hadi watani wao, Yanga ambao imetinga fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwani hadi sasa ina uhakika wa kuvuta Dola 1 Milioni (zaidi ya Sh 2.35 Bilioni, badala ya 1.8 Bilioni zilizokuwa kwenye kiwango cha zawadi cha awali ikimaliza ya pili. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi jioni kwenye mtandao wa CAF, ni kwamba zawadi za msimu huu zimeboreshwa kwa asilimia 40 ikiwa ni utekelezaji wa ratifa zilizowahi kutolewa na Rais wa Shirikisho hilo, Dk Patrice Motsepe mapema mwaka huu juu ya ongezeko hilo. Kwa mujibu wa viwango vya sasa vya zawadi hizo kwa Ligi ya Mabingwa, Bingwa anazoa Dola 4 Milioni (zaidi ya Sh 9.4 Bilioni), huku anayemaliza wa p

Rema, Ayra Starr watishia ufalme wa Diamond Platnumz

Image
Ikumbukwe hata video za Diamond ambazo zimefikisha 'views' milioni 100, hakuna iliyofanya hivyo ndani ya mwaka mmoja ila Rema kafanya hivyo mara nne yake tena kwa miezi 12 tu. Rema ndiye msanii wa kwanza Afrika kufanya hivyo wakati rekodi ya Diamond ni Kusini mwa Jangwa la Sahara tu. Remix ya wimbo huo ambayo Rema kamshirikisha Selena Gomez, video yake iliachiwa Septemba 7, 2022 na ndani ya miezi saba sasa tayari imefikisha 'views' milioni 358. Kwa mwaka 2022 Rema alikuwa ndiye mwanamuziki aliyefanya vizuri zaidi YouTube Afrika wakati Diamond hakuwa hata ndani ya 10 bora!. Rema ndiye alichukua nafasi ya kwanza na ya pili katika orodha ya video 10 zilizotazamwa zaidi YouTube Afrika 2022, video nyingine ni Last Last ya Burna Boy (mil. 140), Buga ya Kizz Daniel (mil. 108) na For My Hand ya Burna Boy (mil. 70). Nyingine ni Finesse ya Pheelz (mil. 61), Emiliana ya Ckay (mil. 57), Ku Lo Sa ya Oxlade (mil. 54), No Wahala Remix ya 1da Banton (mil. 53) na Rush ya Ayra Starr (mil