Posts

Showing posts with the label Diamond Platnumz

Rema, Ayra Starr watishia ufalme wa Diamond Platnumz

Image
Ikumbukwe hata video za Diamond ambazo zimefikisha 'views' milioni 100, hakuna iliyofanya hivyo ndani ya mwaka mmoja ila Rema kafanya hivyo mara nne yake tena kwa miezi 12 tu. Rema ndiye msanii wa kwanza Afrika kufanya hivyo wakati rekodi ya Diamond ni Kusini mwa Jangwa la Sahara tu. Remix ya wimbo huo ambayo Rema kamshirikisha Selena Gomez, video yake iliachiwa Septemba 7, 2022 na ndani ya miezi saba sasa tayari imefikisha 'views' milioni 358. Kwa mwaka 2022 Rema alikuwa ndiye mwanamuziki aliyefanya vizuri zaidi YouTube Afrika wakati Diamond hakuwa hata ndani ya 10 bora!. Rema ndiye alichukua nafasi ya kwanza na ya pili katika orodha ya video 10 zilizotazamwa zaidi YouTube Afrika 2022, video nyingine ni Last Last ya Burna Boy (mil. 140), Buga ya Kizz Daniel (mil. 108) na For My Hand ya Burna Boy (mil. 70). Nyingine ni Finesse ya Pheelz (mil. 61), Emiliana ya Ckay (mil. 57), Ku Lo Sa ya Oxlade (mil. 54), No Wahala Remix ya 1da Banton (mil. 53) na Rush ya Ayra Starr (mil

Lavalava kujiunga na Aftermath Entertainment na kuondoka WCB

Image
Hakuna ubishi kuwa baada ya Mbosso na Zuchu kusainiwa kulipelekea WCB Wasafi kupunguza nguvu kwa baadhi ya wasanii ambao ni Lava Lava na na Queen Darleen. Mathalani ni zaidi ya miaka mitatu sasa Queen Darleen hajatoa wimbo, mara ya mwisho kufanya hivyo ilikuwa Aprili 2020 alipoachia ngoma, Bachela akimshirikisha Lava Lava, huku akiwa hajatoa albamu wala EP chini ya WCB Wasafi. Ujio wa wageni hao wawili hasa Zuchu, kunaweza kutafsiriwa kama kutia mchanga kitumbua cha Lava Lava, mfano Zuchu amekuwa anatoa ngoma mfululizo kuliko msanii yoyote wa WCB Wasafi. Wakati Lava Lava anatimiza miezi tisa bila kutoa ngoma, kwa kipindi hicho Zuchu ameweza kutoa ngoma sita ambazo ni Jaro, Love, Kwikwi, Utaniua, Napambana na Nani. Kwa mwenendo huo huwenda maisha ya Lava Lava sio marefu ndani ya WCB Wasafi, anaweza kuondoka kama ilivyokuwa kwa Harmonize, Rich Mavoko na Rayvanny. Hata hivyo, swali la wengi ni vipi ataweza kupata mafanikio kuzidi yale aliyopata chini ya lebo hiyo? au ataenda kuwa tishio k

Diamond Platnnumz, Alikiba, Harmonize, Sauti Sol Waletewa tuzo zao

Image
  Waandaaji wa Tuzo za Magic Vibes Awards wamezungumza na wana habari leo wakieleza kuleta tuzo kwa wasanii walioshinda baada ya kutangazwa washinndi. Tuzo hizo ambazo zinaanndaliwa nchini Marekani Texas ni maalumu kwa ajili ya wasanii kutoka Afrika Mashariki. Miongoni mwa wasanii walioshiriki ni Diamond Platnnumz, Alikiba, Harmonize, Sauti Sol na wengine.

Kipi kinamkwamisha Lavalava WCB

Image
  Hata hivyo, sasa inaonekana kuna kitu hakipo sawa kwa Lava Lava katika safari yake ya muziki ukilinganisha na wasanii wengine hasa wale waliokuja nyuma yake, Mbosso na Zuchu. Mbosso aliyejiunga WCB Wasafi, Januari 2018, tayari ametoa albamu moja, Definition of Love (2021) na EP moja, Khan (2022), wakati Lava Lava ametoa EP moja tu, Promise (2021). Tayari Mbosso ameshinda tuzo mbili, HiPipo Awards 2019 kama Video Bora ya Mwaka (Hodari) na Tanzania Music Awards (TMA) 2022 kama Msanii Bora wa Kiume wa Bongofleva, ila Lava Lava hajashinda tuzo yoyote. Naye Zuchu aliyetambulishwa WCB Wasafi hapo Aprili 2020 katoa EP moja, I Am Zuchu (2020) sawa na Lava Lava lakini yake ilitoka kwa ukubwa zaidi, ilifanyiwa 'listenig party', huku akitoa video tano wakati ile ya Lava Lava ikitoa video moja tu!. Wakati mwaka huu Zuchu akiandika rekodi kama msanii wa kike Bongo aliyeshinda tuzo nyingi za TMA 2022, tano, Lava Lava hata hakuchaguliwa kuwania, ni yeye na Queen Darleen pekee ndio wasanii w