Hii Hapa ni Jumla ya Fedha Watakazovuna Yanga Baada ya Kuingia fainali
YANGA tayari ipo kwenye fainali za Shirikisho Afrika, baada ya kuwatoa Marumo Gallants ya Afrika Kusini wiki hii. Mabingwa hao wa Tanzania, wamejikakikishia kiasi cha Dola 800,000 (zaidi ya Sh 1.8 Bilioni) kwa kutinga fainali na kama itafanikiwa kuinyoosha USM Alger ya Algeria watakaokutana nao basi, itazoa Dola 2 Milioni (zaidi ya Sh 4.7 Bilioni). Lakini kama unadhani Yanga itavuna kiasi hicho tu, pole yako kwani kwa kubeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa msimu wa pili mfululizo, tayari wababe hao wameshajihakikisha zaidi ya Sh 700 milioni kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo yaani Benki ya NBC na Azam Media. Azam inayodhamini matangazo ya ligi hiyo bonasi zake kwa bingwa wa msimu ni Sh 500 milioni, huku kwa NBC wanatoka Sh 100 milioni ilihali wadhamini wakuu wa Yanga, SportPesa inayoipa klabu hiyo zaidi ya Sh 4 Bilioni kwa mujibu wa mkataba mpya walioingia mwaka jana wenye thamani ya Sh 12 Bilioni kwa miaka mitatu, pia itaipa mabingwa hao Sh 150 Milioni kama bonasi ya ubingwa. Ukiacha fe